Wednesday, 1 April 2015

mwendesha mashtaka uturuki auawa.....

  • Saa 5 zilizopita

Waziri mkuu wa Uturuki, Ahmet Davutoglu

Mwendesha mashtaka wa kituruki ambae alizuliwa mateka katika mahakama moja mjini Istanbul na wapiganaji wenye mrengo wa kushoto amefariki kutokana na majeraha aliyoyapata katika mapigano ya risasi na polisi.
Mwendesha mashtaka huyo ambaye alikuwa anahusika na uchunguzi wa kina, alipigwa risasa mara kadhaa katika operasheni iliyofanywa na vikosi vya uturuki ya kumaliza uvamizi uliodumu kwa siku moja kotini hapo.
Waziri mkuu wa Uturuki, Ahmet Davutoglu, amesema mwendesha mashtaka huyo amepoteza maisha licha ya jitihada za daktari za kumwokoa."Upasuaji ulianza saa mbili na dakika ishirini na tao na ulimalizika katika muda mfupi sana. Mwendesha mashitaka wetu aliumizwa vibaya sana na kukimbizwa hospitalini na nimezungumza na mganga mkuu. Pamoja na juhudi zote hizi,kwa bahati mbaya alipoteza maisha. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya mwendesha mashitaka Mehmet Selim Kiraz." amesema waziri mkuu Davutoglu.
Waziri mkuu Davutoglu amesema baadhi ya taratibu za kiusalama zitaangaliwa upya kutokana na hali ya utekaji. "Wakati tunaangalia majadiliano ambayo yamefanyika hivi karibuni katika muundo wa usalama, tukio hili linafungamanisha usalama na uhuru. Wakati wa mikutano na mazungumzo yetu tumeamua ufanyike uchunguzi wa kina kuhusu tukuio hili na kubaini kasoro za kiusalama. Tumeamuru hatua stahiki zichukuliwe katika siku za baadaye."
Share:

Rais wa Nigeria ni Muhammadu Buhari

Rais mteule was Nigeria Jenerali Muhammadu Buhari
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini Nigeria,INEC, Attahiru Jega amemtangaza rasmi Kiongozi wa wa chama cha upinzani cha Nigeria jenerali Muhammadu Buhari kuwa rais wa taifa hilo kubwa barani Afrika baada ya kumbwaga rais wa zamani Goodluck Jonathan.
Tayari rais anayeondoka madarakani Goodluck Jonathan amekwisha kubali kushindwa kwake baada ya kumpigia simu mpinzani wake, Jenerali Buhari na kumpongeza kwa ushindi huo wa kihistoria.
Hii inakuwa mara ya kwanza katika historia ya taifa hilo kwa rais wa nchi hiyo kung'olewa madarakani na kiongozi wa upinzani.
Goodluck amekiri kushindwa katika uchaguzi huo ulioshuhudia ushindani mkali
Wadadisi wa maswala ya ndani wanasema kuwa inaonekana kuwa Nigeria sasa imekomaa kisiasa haswa baada ya kushuhudia mapinduzi kadha ya kijeshi tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Uingereza mwaka wa 1960.
Hata hivyo kumekuwa na taharuki kubwa haswa baada ya tume ya uchaguzi kuchelewa kutoa matokeo ya uchaguzi.
Hofu ingalipo kuwa huenda wafuasi wa wagombea hao ambao wanatofautia kimsingi katika maswala kadha ikiwemo ya kidini na vile vile kimajimbo .
Wanigeria wengi wamefurahi kushiriki uchaguzi uliomtoa mamlakani raisl aliyekuwa hatekelezi wajibu wake
Wanigeria wengi wamefurahi kuwa hatimaye wameweza kuing'oa mamlakani serikali ambayo haikuwa ikitekeleza majukumu yake kikamilifu.
Buhari angali hajatangazwa rasmi kuwa mshindi na tume hiyo japo alikuwa amefungua pengo la zaidi ya kura milioni tatu dhidi ya mpinzani wake wa karibu rais Goodluck.
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive