Friday, 19 July 2013

WASICHANA WA SEKONDARI NI HATARI SANA KWA SASA TUWE MAKINI


 
Habari wanajamvi. 
Ngoja nami niwe mtoto kidogo kwa kusimulia na kutoka kasiri ka mambo ya kitoto.
 
Wiki iliyopita nilikuwa natoka zangu Mbeya kuelekea Dar es salaam kwa basi moja hivi.
 
Jirani yangu kwenye siti alikuwa amekaa "katoto" flani ka kike kama ka miaka 17-19. 

Yule mtoto alikuwa mstaarabu sana. Akaniamkia kisha akatulia. Gari lilipoondoka akaanza kunisemesha. Akaniuliza ninapokoka, niendako, origin yangu na maswali kibao ya kizushi. Akajitambulisha kuwa yeye ni mwanafunzi wa kidato cha nne alikuwa anaumwa akarudi nyumbani anaelekea shuleni(akataja jina la shule).
 
Njiani nikawa nikinunua maji namnunulia, nikinunua kitu chochote naye namnunulia. Safari ikaendelea.
 
Tulipofika Morogoro akaniomba nimwazime simu yangu afanye mawasiliano kwani yake haina credit. Bila hiyana nikampatia akaitumia akanirejeshea.
 
Kwa kweli nilimchukulia kama mdogo wangu tu hadi tunafika.
 
Kituko kikaanza usiku kama saa 6:30 usiku hivi, nikiwa nimelala ikaingia message kwenye simu yangu "mimi yule dada tuliyesafiri wote leo, umefika salama nyumbani? Usiku mwema".
 
Kumbe katoto ka watu kalichukua namba yangu bila mimi kujua. Basi mtoto akatuma tena asubuhi kama saa 12:00 "vipi umeoa? Unaonekana mstaarabu, nimemiss sana jinsi ulivyo mpole, asubuhi njema".
 
Sikujibu chochote. Mchana akatuma message tena, jioni tena nami bila kujibu. Usiku wa siku ya pili kama saa tano usiku akapiga tena simu na kunitamkia anapenda tukutane aniambie jinsi gani alivyonipenda kimapenzi. Kisha akakata simu nami sikupiga.
 
Jioni nikamtumia message nikimpa ushauri na kumnasihi kuwa ajitahidi katika masomo yake na aache kufikiria kuhusu mapenzi. 

Akakoma kupiga na kutuma tena message ila nikawa nimejifunza kitu kwa zile message alizokuwa anatuma. Utadhani kaandikiwa jinsi zilivyojaa maneno ya kimahaba ya kukata na shoka. Na jinsi message zilivyo huwezi amini kama kaandika mtoto wa sekondari.
 
Kama hali ndo ilivyo kwa mabinti zetu wanaosoma basi kazi tunayo wazazi na 
hatutavuna kitu kwa mabinti zetu wa aina hii.
Share:

SERIKALI YASISITIZA KUWA "KODI YA LINE ZA SIMU" IKO PALE PALE...!!!


Waziri wa Fedha, William Mgimwa, amesisitiza uamuzi wa Serikali kuendelea kutoza Sh 1,000 kwa kila mwezi kwa laini ya simu, licha ya kampuni za simu na wanasiasa kupinga.
Akizungumza na mwandishi juzi, Mgimwa alikumbusha wanaolalamikia kodi hiyo, kwamba suala la ulipaji kodi kwa taasisi au watu binafsi, ni la kisheria kulingana na mapato yao na hali halisi iliyopo.
Pia alieleza kushangazwa na matangazo ya baadhi ya kampuni kuhusu utozwaji kodi wananchi akisema wananchi ndio wanataka barabara, maji na umeme vijijini na kodi hizo zinakwenda kutumika huko. 
Kwa mujibu wa Mgimwa, kodi ya laini za simu na ya intaneti, imetengwa ikatumike kusaidia maji na uwezo wa Serikali kupeleka elimu vijijini jambo ambalo ni la maendeleo.

"Wananchi wenyewe wanalalamikia ukosefu wa huduma na baada ya Serikali kupitia na kufanyia kazi changamoto hizo, imeridhia kodi hizo wanakuja watu wanalalamika," alisema.
  
Alisisitiza kuwa ongezeko la kodi kwa huduma za intaneti, ni kwa ajili ya kuboresha mfumo wa elimu ambao unalalamikiwa mara kwa mara.
Mgimwa alisema ulipaji kodi unatokana na aina ya biashara na mapato na kutaka kampuni zinazokatwa kodi, kutojilinganisha na kampuni zingine.
Alishangaa wabunge wanaolalamikia ulipaji Sh 1,000 za simu, kwa maelezo kwamba kodi hiyo haikupendekezwa na Serikali, bali Bunge kupitia Kamati ya Bunge lilitaka wananchi wakatwe Sh 1,450.
Baada ya mapendekezo, Mgimwa alisema Serikali ilifanya  uchambuzi na kuamua kupunguza hadi Sh 1,000.  
  
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, jana alisema msimamo wa Serikali ndio wake pia.
Kauli ya Mgimwa inajibu malalamiko ya baadhi ya kampuni, wabunge na vyama vya siasa, kwamba ongezeko hilo linaongeza ugumu wa maisha kwa wananchi.
Hivi karibuni kampuni za simu na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), walilalamikia kodi hiyo kwamba inaongeza gharama za maisha kwa wananchi.
Mbali na Mnyika, hata CCM kupitia taarifa ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ilitaka kodi hiyo iondolewe na Serikali itafute vyanzo vingine vya mapato.  
Pia Chama cha Watoa Huduma za Mitandao ya Intaneti Tanzania (TISPA), walilalamikia sheria mpya ya kodi na ushuru wa bidhaa katika intaneti, kwamba itachangia ongezeko la gharama za huduma ya intaneti kwa watumiaji wa kawaida.

Share:

WEMA SEPETU JELA INAMUITA


KUNA kila dalili kwamba mrembo anayetamba kwenye filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ au Madam jela inamwita na anatakiwa kufanya maombi ili kukwepa kifungo maishani mwake.
Hali hiyo inafuatia staa huyo kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine tena Jumatano iliyopita, pale alipopanda katika Mahakama ya Mwanzo ya Kawe jijini Dar kwa kosa la kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni meneja wa hoteli moja iliyopo Kawe Beach jijini Dar, Godluck Kayumbu.
Kabla ya  kupandishwa  kwa ‘pilato’,  staa huyo anayemiliki Kampuni ya Endless Fame alikuwa akisakwa na askari kwa siku kadhaa na kufanikiwa kuwapiga chenga za hapa na pale.

ANASWA AKIFUTURU
Hata hivyo, mbio zake ziliishia ukingoni Julai 16, mwaka huu, alipokamatwa saa mbili usiku akiwa anafuturu na wageni wake nyumbani kwake, Kijitonyama Dar.

MTITI KIDOGO
Askari saba walifika nyumbani kwake wakiwa ndani ya Land Rover ‘difenda’ kwa ajili ya kumkamata, hata hivyo walipata upinzani kidogo kutoka kwa mlinzi wa staa huyo ambaye alikuwa akizuia bosi wake asikamatwe ambapo ilibidi askari hao wakaze msuli na kutuliza mtiti uliokuwa ukitaka kutokea.

WEMA AGEUKA MBOGO, ALALA SELO
Baada askari kumfikia staa huyo, walimtaka kwenda naye kituo cha polisi kwa kutumia difenda walilofika nalo ambapo Wema alipinga na kugeuka mbogo kwa kudai kwamba hawezi kupanda difenda kutokana na hadhi yake.

Pamoja na askari kutaka kumpandisha kwa nguvu, staa huyo alipinga na ikakubaliwa apande gari lake aina ya Audi Q7 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari.
Safari ikaishia Kituo cha Polisi cha Kawe ambako staa huyo aliandikisha maelezo na baada ya zoezi hilo akatupwa selo.

WEMA HAUOZI
Kama lilivyo jina lake, wema hauozi, staa huyo alipata dhamana saa 5 za usiku baada ya kudhaminiwa na msanii  mwenzake wa filamu, Kajala Masanja.
Kajala aliwahi kutolewa katika mdomo wa jela na Wema siku za nyuma baada ya kukutwa na hatia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar alipotakiwa kulipa faini ya shilingi milioni 13 au kwenda jela, Wema alimlipia kiasi hicho cha fedha.
WAPAMBE FULL SHANGWE
Wapambe wa Wema waliokuwa wamejazana nje ya kituo hicho cha polisi, walilipuka kwa shangwe baada ya bosi wao kuchomolewa kutoka selo. Staa huyo aliondoka na gari lake lililokuwa likiendeshwa na meneja wa kampuni yake aitwaye Petit Man.

ATEMBEZWA KWA MIGUU
Julai 17, asubuhi Wema alirudi kituoni hapo na kuwekwa chini ya ulinzi kwa ajili ya kupelekwa mahakamani kusomewa mashitaka yake.
Katika hatua ya kushangaza, staa huyo alitembezwa kwa miguu umbali wa mita 200 kutoka kituo cha polisi hadi Mahakama ya Mwanzo ya Kawe.
APANDISHWA KIZIMBANI
Wema alipandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake na Mh. Hakimu, Bernice Ikanda na kudaiwa kufanya vurugu, kushambulia kwa kumpiga makofi na kumtukana Kayumbu.
Mbele ya hakimu, Wema alikana mashitaka na hakimu aliiahirisha kesi hiyo mpaka Julai 31, mwaka huu.

IKO SIKU WEMA ATAFUNGWA GEREZANI
Kumbukumbu kutoka kwenye makabrasha yetu zinaonesha kuwa, mrembo huyo ni mtu wa majanga, mara kwa mara amekuwa akifikishwa polisi na mahakamani kutokana na ugomvi.

ALIVUNJA KIOO CHA GARI LA KANUMBA
Mwaka 2009, Wema alidakwa na Polisi Kituo cha Magomeni na baadaye kupandishwa katika Mahakama ya Kinondoni, Dar kwa Hakimu Emilius Mchalu kwa kosa la kuvunja kioo cha gari la aliyekuwa staa wa filamu za Kibongo, Marehemu Steven Kanumba chenye thamani ya shilingi milioni moja. Hata hivyo, Kanumba aliifuta kesi hiyo.

ALIMTISHIA MAISHA BOB JUNIOR
Kama vile haitoshi, mwaka 2011, Wema huyohuyo alikamatwa na Polisi wa Oysterbay jijini Dar na kufikishwa Mahakama ya Mwanzo, Kinondoni kwa kosa la kumtusi na kumtishia maisha mwanamuziki wa Bongo Fleva, Rahem Nanji ‘Bob Junior’.
Katika kesi hiyo, Hakimu Mariam Masamalo alimtia hatiani Wema kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi 40,000 ambapo alilipa fedha hizo.
ALIMTUSI REHEMA FABIAN
Aidha, mara baada ya Wema kuachiwa huru mahakamani hapo alikamatwa tena na polisi kwa kile kilichodaiwa kumtusi Miss Kiswahili 2008, Rehema Fabian. Wema alipelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar kwa maelezo zaidi.

ALIMTUKANA MSANII
Aidha, Wema amewahi kulala kituo cha Polisi Oysterbay, Dar akiwa na mashoga zake, Kajala na Dida kwa madai ya kumshambulia mwigizaji mmoja wa Bongo, kwenye pati iliyofanyika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar. Kesi hiyo iliisha kwa mazungumzo nje ya polisi.
Imeandikwa na Musa Mateja, Mwaija Salum, Makongoro Oging’ na Shakoor Jongo.
Share:

mzee wa miaka 63 atupwa jela miaka 30 kwa kosa la kumbaka binti wa miaka 16 ndani ya msikiti,,,



Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma, imemhukumu Ahamad Fadhil (63), kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na kosa la kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 16 ndani ya Msikiti wa ni Mwembe Mmoja, mjini hapa.

Hukumu hiyo ilitolewa na jana na Hakimu wa mahakama hiyo, Obadiah Bwegoge, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa.

 

Hakimu Bwegoge alisema mahakama hiyo inatoa adhabu kali dhidi ya mshtakiwa huyo ili liwe fundisho kwake na kwa vijana wengine wenye tabia ya kikatili kama yake.

 

  Alisema upande wa mashitaka ulipeleka mahakamani hapo mashahidi watano ambao bila kuacha shaka, walithibitisha kuwa mshtakiwa huyo alimbaka msichana huyo (jina limehifadhiwa) na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

 

 

Alisema shahidi wa kwanza upande wa Jamhuri ambaye ni mlalamikaji, alidai kuwa siku ya tukio, saa nane 8:00 mchana, alikwenda msikitini hapo kuomba msaada kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kifafa.

 

 “Nilipofika nilikutana na huyo baba akaniambia ni kiongozi wa msikiti, hivyo nilisubiri akanichangishie fedha kwa waumini wake,” alidai.

 

  “Ndipo mimi nikaingia ndani ya msikiti upande wa wanawake kuswali, baada ya kumaliza kuswali, mzee huyo aliniita na kuniingiza ndani ya eneo lingine nikafikiri nakwenda kuchukua mchango, kumbe nakwenda kubakwa,” alidai msichana huyo mahakamani.

 

 

  Alidai kuwa mshtakiwa alimpapasa sehemu mbalimbali za mwili wake na kwamba alijitahidi kukataa lakini aliishiwa nguvu na ndipo mshtakiwa alipotumia fursa hiyo kumwangusha chini na kuanza kumbaka. Temblea machemba.blogspot.com kila siku.

 

  Kwa mujibu wa msichana huyo, wakati tukio hilo likiendelea, alitokea mzee mwingine na kuwatenganisha na mshtakiwa wakati akiendelea kumbaka.

 

  “Alimtoa juu yangu na huyo baba ambaye ni mshtakiwa na kuanza kukimbia, ndipo waumini wa msikiti huo walipomkimbiza na kumkamata na kuanza kumpa kipigo,”alidai.

 

  Alidai kwmaba wakati huo alikuwa amezimia na kwamba alipozinduka alijikuta akiwa wodini katika Hospitali ya Mkoa Maweni.

 

  Mshtakiwa alipopewa fursa ya kujitetea, aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa madai kwamba  waumini wenzake wanamchukia ndiyo maana walinimpeleka mahakamani.

 

 

Kadhalika, alidaim kuwa sehemu zake za siri hazifanyi kazi kwa muda mrefu hivyo alisingiziwa.

 

  Hakimu Bwegoge alitupilia mbali utetezi huo na kumhukumu kifungo cha miaka 30 jela.

 

 

Awali, ilidaiwa  na Mwendesha Mashitaka Inspekta wa Polisi, Athumani Mshana, kuwa Febuari 19, mwaka huu, saa 8:00 mchana, eneo la Ujiji, Manispaa ya Kigoma/Ujiji, mshtakiwa alimbaka msichana mwenye umri wa miaka 16 ndani ya msikiti wa Mwembe Mmoja baada ya swala ya adhuhuri na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za

Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive