Tuesday, 1 October 2013

Bayern na mtihani dhidi ya Manchester City

Kocha wa Bayern Pep Guardiola atakabiliwa na mtihani mwingine dhidi ya timu ya premier League, katika Champions League baada ya kupata ushindi wa kombe la Super Cup dhidi ya Chelsea kupitia mikwaju ya penalti 
 
 
Mlinda lango wa Bayern Manuel Neuer anasema huu utakuwa mchuano wa timu mbili zenye nguvu sawa, wakati naye nahodha wa Manchester City Vincent Kompany akiwataka wenzake wakaze buti baada ya kichapo cha mabao matatu kwa mawili dhidi ya Aston Villa.
Katika kundi F, Arsenal ambao maisha yao yanaonekana kuwa ya starehe wakati wakiongoza Ligi Kuu ya England, watakuwa wenyeji wa Napoli. Timu zote mbili zilishinda mechi zao za kwanza za Champions League.
Nao Borussia Dortmund wana mchuano wa nyumbani dhidi ya Olympique Marseille. Baada ya kichapo cha nyumbani cha mabao mawili kwa moja na West Bromwich Albion Jumamosi iliyopita katika Ligi ya nyumbani, mbinyo unazidi kuongezeka dhidi ya kocha wa Manchester United David Moyes kabla ya mpambano wao wa Jumatano ugenini na Shakhtar Donetsk katika kundi A
 
Kevin Prince Boateng ameongeza makali katika ushambuliaji wa Schalke tangu alipojiunga nao msimu huu
kevin Prince Boateng ameongeza makali katika msimu huu ushambuliaji wa Schalke tangu alipojiunga nao
 
 AC Milan inawakaribisha tena kikosini Riccardo Montolivo na Stephan El Shaarawy baada ya kupona majeraha yao pamoja na Mario
 Balotelli ambaye amepumzika vya kutosha, wakati watakapochuana na Ajax mjini Amsterdam katika mechi ya kundi H hapo kesho. Barcelona watasafiri mjini Glasgow kupambana na Celtic hapo kesho katika mechi ya kundi H, bila ya huduma za mashambuliaji wao Lionel Messi. Muargentina huyo alipata jeraha katika mguu wake wa kulia mwishoni mwa wiki lakini Neymar yuko tayari kulijaza pengo hilo.
Atletico Madrid watasafiri hadi Porto katika mchuano wa kundi G. Real Sociedad watajaribu kujikwamua ugenini dhidi ya Bayer Leverkusen katika mechi ya kundi A. Schalke wa Ujerumani wako na kibarua dhidi ya Basel katika mechi ya kundi E, baada ya timu hiyo ya Uswisi kubwaga Chelsea mabao mawili kwa moja katika mchuano wa kwanza nao Schalke wakawapiku Steaua Bucharest mabao matatu bila jawabu. Sasa kocha wa Chelsea Jose Mourinho anasema Juan Mata ataanza katika mchezo wa kesho dhidi ya Steaua ambao ni lazima aishinde. Katika kundi C, Paris St Germain watapambana na Benfica nao Anderlecht wakiwaalika Olympiakos siku ya Jumatano.
Share:

Kenya yawaombea wahanga wa shambulizi la Westgate

Ni siku 9 sasa tangu mkasa wa Shambulizi la magaidi kutokea katika Jumba la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, Kenya. Serikali imeandaa maombi ya kitaifa yanayojumuisha dini zote kuombea usalama wa nchi 
  Maombi hayo pia ni ya kuwafariji wale waliopoteza wapendwa wao kwenye shambulizi hilo la magaidi lililosababisha vifo vya watu 67 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa.
Viongozi wa dini mbali mbali wamekusanyika katika uwanja wa jumba la KICC kwa maombi ya kitaifa kuombea nchi, manusura na jamaa za waliopoteza wapendwa wao kwenye shambulizi la magaidi Shambulizi hilo lililofanyika tarehe 22 mwezi huu. Maombi hayo yamehudhuriwa na wakuu wa serikali wakiongozwa na Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Rutto, mawaziri na wabunge.
 Bado kuna maswali mengi yaanyostahili majibu kuhusu namna serikali ilivyolishughulikia shambulizi hilo
 Bado kuna maswali mengi yaanyostahili majibu kuhusu namna serikali ilivyolishughulikia shambulizi hilo

Pia viongozi wa upinzani wa muungano wa CORD wakiongozwa na aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga akiandamana na viongozi wa vyama tanzu wa muungano huo, aliyekuwa makamu wa Rais Kalonzo Musyoka na wengineo walijumuika pamoja katika uwanja wa jumba la mikutano ya Kimataifa KICC.
Maombi hayo yanahudhuriwa na viongozi wa didi mbali mbali wakiwemo wakristo, Waislam, 
Wahindu na dindi nyinginezo. Viongozi wa dini ya kiislam wameendelea kukikashifu kitendo 
 hicho cha magaidi na kusihi vyombo vya usalama kutohusisha ugaidi na Uislam.. Huku maombi hayo yakiendelea kundi la wataalam wa uchunguzi kutoka mataifa mbali mbali wanaendelea na uchunguzi wao katika jumba la Westgate Mall kutafuta ushahidi kuhusiana na shambulizi hilo. Maafisa kutoka Uingereza, Ujerumani Marekani, Israel na Canada wakishirikiana na wenzao kutoka Kenya wanaendesha shughuli iliyoanza Jumatano iliyopita. Maswali mengi hadi sasa hayajapata majibu kuhusiana na shambulizi hilo lililodaiwa kuteklelezwa namagaidi wa kundi la Al-Shabaab walio na uhusiano na kundi la magaidi la Al-Qaeda. Washukiwa tisa bado wanahojiwa na polisi kuhusian na shambulizi hilo. Serikali imesema magaidi 5 waliuawa kwenye shambulizi hilo ingawaje hadi sasa hakuna hata maiti moja ya magaidi hao iliyotambuliwa.
Share:

Shughuli za serikali ya Marekani zaanza kufungwa

Sehemu kubwa ya shughuli za Serikali ya Marekani zimefungwa leo baada ya wabunge wa nchi hiyo kushindwa kuutatua mgogoro wa bajeti. Hali hiyo imetokea kwa mara ya kwanza baada ya miaka 17 
Malaki ya watumishi wa serikali wanarudishwa nyumbani bila ya malipo na idara nyingi za serikali zimeambiwa zifunge milango. Sehemu kubwa ya shughuli za serikali ya Marekani zimefungwa kwa sababu serikali hiyo haina bajeti ya matumizi ya kawaida. Mgogoro huo maana yake ni kwamba wafanya kazi wa serikali kuu hadi milioni moja watapewa likizo bila ya malipo.
Baadhi ya huduma za umma kama vile miradi ya utafiti wa tiba zinazoendeshwa na idara za serikali pia zitasimama. Marekani imefikia hatua hiyo baada ya baraza la seneti linalodhibitiiwa na chama cha Rais Obama cha Demokratik kulikataa pendekezo la wajumbe wa chama cha Republican la kuusimamisha mpango wa huduma za afya wa Rais Obama.
Wabunge wa chama cha Republican wanaolidhibiti baraza la wawakilishi walitaka mchakato wa nipe nikupe na chama cha Demokratik. Wabunge wa Republican walikuwa tayari kuipitisha bajeti lakini kwa sharti la kuusimamisha mpango wa afya wa Obama ambao umeanza kutekelezwa leo.
Mpango wa Rais Obama wa huduma za afya kwa Wamarekani unavurugwa na wabunge wa Republican 
 Mpango wa Rais Obama wa huduma za afya kwa Wamarekani unavurugwa na wabunge wa Republican

Juu ya kufungwa kwa shughuli za serikali Rais Barack Obama amesema. "Kwa bahati mbaya bunge halikuutimiza wajibu wake." Hata hivyo baadhi ya wizara zitaendelea kufanya kazi kama vile ya ulinzi. Rais Obama aliwatumia wanajeshi ujumbe wa video kwa kusema. "Kama amirijeshi wenu nimehakikisha kwamba mtaendelea kuwa na uwezo, zana na yote mnayoyahitaji ili kuutekeleza wajibu wenu kwa taifa. Vitisho kwa taifa letu bado havijabadilika na hivyo tunawataka muwe tayari kwa dharura yoyote"

Kila upande unaulaumu mwingine kwa kushindwa kufikiwa kwa makubaliano. Rais obama ametahadhrisha juu ya madhara ya kiuchumi yanayoweza kutokea kufuatia kusimamishwa kwa shughuli za serikali. Amesema kasi ya ustawi wa uchumi inaweza kuvurugika.
Hatua iiyofikiwa leo pia inasababisha wasi wasi iwapo Marekani italifikia lengo lake hadi kati kati ya mwezi wa oktoba la kuongeza deni la serikali hadi dola Trilioni 16.7. Hisa barani barani Ulaya zimepanda juu kidogo mapema leo lakini wawekaji vitega uchumi wameingiwa wasi wasi.
Hata hivyo wachunguzi wanaamini kuwa wabunge wa Marekani watakaa chini pamoja haraka ili kutafuta ufumbuzi. Licha ya kuwa suala muhimu kwa masoko, madhali pana matumaini, masoko hayataathirika sana. Hayo ameyasema mtaalamu wa masuala ya fedha wa Unicredit mjini Munic, Christian Stocker. Wakati huo huo uchunguzi wa maoni umeonyesha kuwa chama cha Republican kitalaumiwa na wananchi wengi wa Marekani kwa kufungwa kwa shughuli za serikali.
Share:

MWANAMKE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUMTUPA MTOTO WAKE CHOONI

 
 Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni. Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo. 

Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa.


Ameongeza kuwa amelazimika  kutupa katika choo cha jirani kwa sababu ni cha shimo tofauti na chao ambacho asingeweza kutupa mtoto huyo.

Rukia Haruna (31)  akitolewa nje  na Askari wa Jeshi la Polisi akitolewa nje ya  Mahakama kwenda Gerezani kutumikia kifungo cha miaka 5 Jela  

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Zabibu Mpangula, amemtaja Mtuhumiwa kuwa ni Rukia Haruna (31) mkazi wa Manga A Jijini Mbeya na kwamba kosa lake ni kinyume cha kifungu  218 kifungu kidogo cha 35 sura ya 16 ya mwaka 2002.
 
Share:

GAIDI WA KIKE WA AL SHABAAB SAMANTHA KATIKA MAPOZI MBALI MBALI YA KICHOKOZI


Samantha Louise Lewthwaite, (born 5 December 1983), also known as Sherafiyah Lewthwaite or the White Widow, is the widow of 7/7 suicide bomber Germaine Lindsay and one of the United Kingdom's most wanted terrorism suspects She is currently a fugitive from justice in Kenya, where she is wanted on charges of possession of explosives and conspiracy to commit a felony and is the subject of an Interpol Red Notice requesting her arrest with a view to extradition. Below are some photos of her

 
 
Share:

Mancini kwenda Uturuki


Kocha wa zamani wa Manchester City ,Roberto Mancini anazungumza na mabingwa wa Uturuki Galatasaray kuhusu nafasi iliyo wazi ya kocha wa klabu hiyo. 
kocha wa zamani wa klabu ya manchester city
Roberto mancini
Mancini alifutwa kazi Manchester City

Klabu hiyo ya mjini Istanbul ilithibitisha katika mtandao wa Twitter kwamba Mancini amekutana na wakurugenzi wa klabu hiyo na kupigwa picha na mkurugenzi mkuu , Lutfi Aribogan.
Mtaliana huyo anatarajiwa kushika nafasi ya Fatih Terim, ambae alipigwa kalamu wiki iliyopita baada ya kushindwa kukubaliana mkataba mpya.
Manchester City ilimfuta Mancini mnamo mwezi wa Mei mwaka mmoja baada ya kuongoza hadi kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya England.
Galatasaray imeanza vibaya msimu wa soka Uturuki ikishinda mechi moja tu kati ya michuano mitano ya kwanza .
Katika michuano ya klabu bingwa ya Ulaya ilicharazwa na Real Madrid,kwa mabao 6-1.
Terim, mwenye umri wa miaka 60, aliongoza Galatasary kushinda mara 6 ubingwa wa Uturuki pamoja na kombe la UEFA mwaka 2000 baada ya kuichezea kwa kipindi cha miaka 11.
Mancini ameshinda ubingwa wa Italia mara tatu akiwa na Inter Milan ya Utaliana kabla ya kunyakua kombe la FA na ubingwa wa ligi na Manchester City.
Share:

Wabunge, Kenya - wakimbizi waondolewe !





Kamati ya bunge inayohusika na ulinzi na uhusiano na mataifa ya kigeni imependekeza kufungwa kwa kambi za wakimbizi nchini Kenya, ikisema zinatishia usalama wa nchi.Kambi ya wakimbizi ya Dadaab, Kenya.
 Kambi ya wakimbizi ya Dadaab, Kenya

Mwenyekiti wa kamati hiyo Ndungu Githinji amesema kuwa wana habari kuwa kambi zilizoko kwenye mipaka ya Kenya hutumika kuwapa mafunzo wapiganaji wa kiislamu.
Kenya inahifadhi wakimbizi wa kisomali zaidi ya nusu milioni katika kambi za Dadaab zilizoko kwenye mpaka na Somalia.
Mwenyekiti huyo Ndungu Githinji ameambia BBC kuwa miaka 22 imetosha kwa usaidizi kwa wasomali hao na wanastahili sasa kurudi nyumbani baada ya amani kurejeshwa nchini mwao.
''Hawa wakimbizi wamekaa miaka ishirini na mbili Kenya. Ningependa kuuiomba UN ifunge kambi hizo. Iwarudishe wasomali kwao, maana sasa nao pia wanayo serikali yao. Ili tuweze kukaa kwa amani.''Amesema bwana Githinji.

Lazima usalama uimarishwe

Bwana Githinji pia ametoa wito kwa vyombo vya usalama kuzidisha usalama na doria katika maeneo yanayotishiwa kushambuliwa na Al shabaab.
''Tunasikia AL shabaab wanasema kwamba bado wanataka kutupiga. Naomba kuwa zile sehemu zote walizotoshia kushambulia zipewe ulinzi wa kutosha kwa saa ishirini na nne.''
Wanamgambo wa Alshabaa wamekuwa wakijihusisha na waislamu katika harakati zao huku wakidai kuwa wanapigania haki ya dini ya kiislamu nchini Somalia na hata mataifa jirani kama vile Kenya.
Pia wamekuwa wakilenga Kenya kwa mashambulio kufuatia hatua ya Kenya kuingia nchini Somalia mwaka wa 2011 kuwaondoa wanamgambo hao kwa madai kuwa wanatishia usalama wa nchi.
Kutokana na hilo wabunge waliozuru eneo la shambulio kule Westgate wamefurahishwa na hatua ya waislamu nchini Kenya kujiepusha na kundi hilo la AL-Shabaab.
Mwenyekiti Githinji asema, '' Ningependa kupongeza viongozi wa waislamu ambao wametoa taarifa yao kuwa hawaungi mkono mashambulio haya.''
Mwandishi wa BBC jijini Nairobi anasema kuwa wito huu wa kufungwa kwa kambi za wakimbizi za Dadaab na Kakuma, zimekuwepo kwa muda. Wakenya wengi wanahisi kuwa Kuwepo kwa wakimbizi hao kumeendelea kuiweka nchi hiyo katika hatari ya mashambulio. Lakinim bali na hilo.
Pia baadhi wanahisi wakimbizi hao ndio wa kulaumiwa kwa kupanda gharama ya makaazi hasa katika maeneo ya Nairobi kama vile Eastleigh, wanakoishi kwa wingi zaidi.

Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive