Saturday, 22 June 2013

Watu 6 wauawa Kaskazini mwa Kenya

Watu sita wameuawa kufuatia mapigano mapya ya kiukoo katika kuanti za Mandera na Wajir Kaskazini mwa Kenya.
Ramani ya Kenya

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Kenya, watu wanne waliuawa, wakati wapiganaji kutoka kwa jamii ya Degodia waliposhambulia lori moja ya mizigo.

Gavana wa Jimbo wa Mandera Ali Roba, watu hao waliuawa hiyo jana na emeongeza kusema kuwa wamepokea ripoti kuwa watu hao waliuawa kinyama.

Mandera County governor Ali Roba said the people were killed during the broad daylight attack on Friday.

Roba amesema watu waliokuwa wakisafiri kwa lori hilo waliviziwa katika eneo la Eldas ambapo wanne waliuawa papo hapo na wengine wanne walifanikiwa kutoroka.

Baada ya kuwauawa watu wao, wavamizi hao waliteketeza lori hilo baada ya kupora mali yote.

Shirika la Msalaba Mwekundi nchini Kenya, waliojeruhiwa wanaendelea kutibiwa katika hospitali ya wilaya ya Mandera.

Katika tukio lingine watu wengine wawili wameuawa katika Kaunti ya Wajir.

Gavana wa eneo hilo amethibitisha tukio hilo na kutoa wito kwa raia wa eneo hilo kudumisha amani.

Mashambulio katika eneo la Kaskazini mwa Kenya yamekuwa yakiongezeka katika miezi ya hivi karibuni, tangu serikali ya Kenya ilipoamua kutuma wanajeshi wake nchini Somalia kupambana na wapiganaji wa Al Shabaab.

Tarehe kumi na moja mwezi huu, watu sita waliuwa kufuatia mapigano hayo ya kiukoo katika jimbo la Mandera

Share:

Gari lililomsafirisha Mandela liliharibika

Gari la wagongwa lililokuwa likimsafirisha hospitalini rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela wiki mbili zilizopita, liliharibika likiwa njiani kwenda hospitalini.
Mandela akiwa na Mkewe Graca

Msemaji wa rais wa Afrika Kusini Mac Maharaj, amethibitisha kuwa gari hilo lilikumba na matatizo na kuwa ilibidi rais huyo wa zamani kuhamishwa hadi gari lingine.

Hata hivyo Bwana Maharaj, amesema tukio hilo halikuwa na tishio lolote kwa afya ya Bwana Mandela, kwa sababu alikuwa na madaktari wa kutosha.

Shirika la habari la Marekani CBS limenukuu vyanzo kadhaa vikidai kuwa Mandela alisalia katika eneo hilo kwa zaidi ya dakika arubaini kabla ya usaidizi kufika.

Shirika hilo la CBS limesema kuwa wakati Bwana Mandela alipokuwa akihamishwa hadi gari lingine viwango vya joto vilikuwa chini sana.
Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alikuwa akisafirishwa kutoka hospitali moja mjini Johannesburg hadi Pretoria, wakati wa tukio hilo lililotokea tarehe nane Juni mwaka huu.

Mandela alilazwa hospitalini huku hali yake ikiwa mbaya kutokana na maambukizi ya mapafu ya mara kwa mara na tangu wakati huo amekuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Hii ni mara ya tatu kwa Bwana Mandela kulazwa hospitalini mwaka huu.

Share:

ANGALIA PICHA ZA BOB JUNIOR AKIPEWA KICHAPO LOCATION...!!!

Bob Junior ameshare picha hizi kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika: Kwa Dizaini hii lazima nirudi kwetu k…Aaaaah Maisha Haya Ya Bongo?,,,,COMING SOON Huu Mzigo…1 Love.


Bob Junior akiwa location kushoot video yake mpya, duuuuuuh...!!! kaaazi kweli kwelii

Share:

HII NI KAULI YA FREEMAN MBOWE ALIPOJISALIMISHA POLISI LEO

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na mandeleo Mh. Freeman Mbowe na mbunge wa jimbo la Arusha Godbless Lema wamejisalimisha kwa jeshi la polisi huku wakiendelea kusisitiza kuwa ushahidi walio nao hawatauwasilisha kwa jeshi la polisi mpaka pale rais Jakaya Kikwete atakapounda tume huru ya majaji ya uchunguzi

Share:

MBUNGE WA MBEYA AMTUKANA WAZIRI MKUU NA KUDAI KUWA "TANZANIA HAIJAWAHI KUWA NA WAZIRI MKUU MPUMBAVU KAMA ....."

Katika hali yakushangaza , mbunge wa mbeya mjini kwa tiketi ya CHADEMA, mh. SUGU ameporomosha tusi zito kwa waziri mkuu wa tanzania ( mh. PINDA ) akidai kuwa Tanzania haijawahi kuwa na waziri mkuu mpumbavu kama yeye.....

Tusi la Sugu limekuja baada ya waziri mkuu kuwaruhusu rasimi polisi kutumia nguvu ya ziada kuwadhibiti wananchi kwa kuwashushia kichapo ili wazitii sheria.....

Hili ndo tusi la mbuge wa mbeya kwa waziri mkuu...


Share:

MEYA AZIMIA BAADA YA KUPIGWA NA POLISI

Meya wa Mji Mkuu wa Kampala nchini Uganda akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhumza za kusababisha vurugu.

Kampala, Uganda. Watu wawili wameuawa kwa risasi nchini Uganda juzi, wakiwa katika mkusanyiko kwenye eneo la soko la Kisekka.

Meya wa mji mkuu wa Uganda, Kampala, Erias Lukwago, pia alizirai baada ya kupigwa na polisi hao waliofyatua risasi za mipira kuutawanya umati wa wafuasi wake.

Akiwa kitandani, Meya huyo amesema baada ya kupata kipigo hicho alipoteza fahamu na kukimbizwa hospitalini.

“Bomu ambalo lilinifanya nipoteze fahamu lilirushwa katika gari langu na kuingia ndani,” amesema.

Meya huyo ni mpinzani wa rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni, alieleza kwamba maofisa wa polisi walimpiga kifuani na kuzirarua nguo zake wakimtuhumu kwa kuchochea ghasia.

Katika tukio hilo, imedaiwa kwamba mtu mmoja anadaiwa kufariki dunia na wengine kadhaa kukamatwa wakati wa ghasia hizo.

Hata hivyo, polisi wamekanusha madai ya kumpiga meya huyo, ambaye pia ni mkosoaji mkubwa wa Rais Museveni.

Upinzani umesema kuwa serikali inajaribu kukandamiza kilio cha mageuzi nchini humo.

Katika tukio lingine, kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye alikamatwa kwa kuandaa mkutano ambao polisi hawakuuidhinisha.

Lukwago, juzi alikuwa anaelekea kwenye jopo maalumu kwa mara ya kwanza, ambako huenda ikamwondolea wadhifa wake kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi.


Polisi walizingira nyumba yake na kisha kumpeleka ambako jopo lilikuwa linaendesha vikao vyake.

“Walinipiga kifuani na kudai kuwa nachochea ghasia, walinirarulia nguzo zangu na kunitesa, nilijaribu kuwaambia waniache lakini sikufanikiwa,’’ amesema Lukwago.

Share:

ALICHOKIANDIKA ZITTO KABWE KUHUSU KAULI YA PINDA KURUHUSU POLISI KUPIGA WANANCHI

Baada ya mh.waziri mkuu mizengo pinda kutoa ruhurusa kwa polisi kupiga wananchi..Mh mbunge zitto kabwe nae atoa lake juu ya mh.waziri mkuu…Kupiitia tweet yake Zitto alisema “Viongozi wa kisiasa lazima wajue kuwka akiba ya maneno yao .kuropoka hovyo hovyo wakati kama huu wenye taharuki ni hatarii sana”..Aliongezea “Ni lazima viongozi wawajibishwe kwa maneno wanayotamka.Mh. Pinda anahamasisha ukiukwaji wa katiba na sheria Asipowajibishwa.”

 HIZI NDIZO TWEET ZA MH.ZITTO KABWE


Share:

NKAMIA AZUA VURUGU TENA BUNGENI SAFARI HII ATAKA KUMPIGA MBUNGE MWENZAKE...!!!


Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), kwa mara nyingine ameingia katika kashfa nzito akituhumiwa kutaka kumpiga Mbunge wa Viti Maalumu CUF, Moza Abeid ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Tukio hilo lilitokea mwanzoni mwa wiki ambapo imeelezwa kuwa Nkamia mbali na kutaka kumpiga mbunge huyo, pia alimtolea matusi mazito ya nguoni (gazeti hili haliwezi kuandika).

Kwa mara ya kwanza mbunge huyo aliingia katika kashfa baada ya kutoa kauli bungeni kuwa hazungumzi na mbwa, bali anazungumza na mwenye mbwa kabla ya kuingia katika mzozo na wahariri na baraza la habari aliposema kuwa Jukwaa la Wahariri na Baraza la Habari ni NGOs za kutafuta fedha.

Uchunguzi wa Mwananchi ambao umethibitishwa na Nkamia mwenyewe umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni kutokana na kuzomewa kwa Nkamia katika kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Dalai Wilaya ya Chemba.

Kwa mujibu wa wabunge mashuhuda ambao waliliona tukio hilo, ilielezwa kuwa Nkamia, ambaye pia ni mwandishi wa habari, alianza kumshushia matusi Moza wakiwa ndani ya Bunge hadi walipotoka nje alimfuata na kutaka kumpiga.
"Kweli pale jamaa yetu, alitia aibu, hata hivyo kusema kuwa alikuwa amelewa siyo kweli maana mimi namfahamu Nkamia vizuri ila ilikuwa ni hasira tu," alisema mmoja wa wabunge walioamua ugomvi huo.
Akizungumzia tukio hilo Moza, alisema kuwa wakati akitoka nje ya ukumbi, alipita karibu na kiti anachokaa Nkamia na ghafla akaitwa, lakini akashangazwa na kitendo cha kuanza kurushiwa matusi.

"Kweli Nkamia na mimi tunatoka wilaya moja, lakini siku ile nilishangaa alinitukana matusi ya nguoni kabisa ......... (anayataja), lakini mimi kule sikusema kitu hadi nilipotoka nje alinifuata na mimi hasira ilinishika nikaanza kumjibu akatupa vitabu ili aje anipige wabunge wenzake wakamkamata," alisema Moza.
Alisema kuwa chanzo cha matusi hayo ilikuwa ni tuhuma kwamba Nkamia alimtuhumu Moza kuwa aliandaa vijana katika Kata ya Dalai wakati wa kampeni za uchaguzi wa udiwani ili wamtukane.

"Hata hivyo, waliomwambia hivyo kwamba niliandaa vijana au nilimtukana walimdanganya kwani mimi wakati huo nilikuwa bungeni, lakini yeye ndiye aliyeniporomoshea matusi katika kampeni hizo na ushahidi wa sauti ninao," alisisitiza Moza.

Kwa upande wake Nkamia, ambaye kabla ya kuwa mbunge alikuwa mtumishi wa Serikali katika Shirika la Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) alikiri kutokea kwa tukio hilo, lakini alikanusha kuingia bungeni akiwa amelewa kama ilivyoaminika na watu.
Nkamia alitoa sababu za ugomvi huo kuwa ni kutokana na taarifa kuwa Moza aliandaa kikosi cha vijana wahuni kulishambulia gari la Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuwazomea viongozi wake akiwemo yeye.
Share:

MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGELI WA MIAKA 17 HUKO KIMARA....AVULIWA UCHUNGAJI, MKEWE AOMBA TALAKA...!!!

HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.
Akizungumza nasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.

MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.

Aliendelea kudai kuwa, mtoto alipofikisha mwaka mmoja na miezi nane, walishauriana watafute hausigeli ili mama huyo afanye biashara ya kuwaongezea kipato.
Mama mchungaji alisema alimpata Sessy akiwa na miaka 15, mkazi wa Mbozi, Mkoa wa Mbeya.
Alisema yeye alianza biashara ya genge maeneo ya Kimara-Mwisho ambapo alikuwa akiwahi sokoni saa 11:00 alfajiri na kumwacha msichana huyo akiendelea na kazi za nyumbani.

VISA VYAANZA
Mama mchungaji aliendelea kudai: Baada ya miezi michache, mchungaji alibadilika tabia, alikuwa mkali, wakati mwingine alinifuata sokoni na kunipiga akinishutumu nina uhusiano na wanaume ndiyo maana nachelewa kurudi nyumbani.

MUMEWE AMFICHULIA SIRI
Akadai: “Siku moja mchungaji alinifichulia siri kuwa hausigeli wetu ni mjamzito na mimba ilikuwa yake hivyo akataka iwe siri kati yetu watatu.”

Mama Mariki alisema alikubaliana na mumewe ambapo alivumilia kwa kipindi kirefu lakini uzalendo ulimshinda baada ya msichana huyo kuwa na tabia ya kuwatesa watoto huku akisema aachwe kwani ni mjamzito.

MKE NAYE AFICHUA SIRI
Alisema kuwa baada ya kuona mumewe anamjali zaidi hausigeli kuliko yeye na watoto aliamua kwenda kutoa siri kwa wasimamizi wa ndoa, wakaitwa na kusuluhishwa ambapo waliamua kuwa msichana huyo arudishwe nyumbani kwao Mbeya jambo ambalo mtumishi huyo wa Mungu alilitekeleza, yeye mwenyewe alimrudisha msichana huyo kwao.

NDOA YATIBUKA
Mwanamke huyo alidai mumewe huyo aliporudi Dar, alianza visa akisema kuwa hausigeli alikuwa akimpa ‘mambo’ kuliko yeye ambaye amezeeka huku vitisho na vipigo vikiongezeka maradufu!
“Wasimamizi wa ndoa walituita kwa mara nyingine wakatusuluhisha lakini tulipofika nyumbani, mateso yakawa palepale ndipo wasimamizi waliponiambia nirudi kwa wazazi wangu kwani ni aibu kubwa kwa mtumishi wa Mungu kufanya vile,” alisema na kuongeza:
“Kweli nilirudi kwetu Moshi, wazazi wangu walimpigia simu mume wangu kuhusu matatizo yetu, lakini aliwajibu hanitaki na ataniletea talaka nyumbani.”
Alisema miezi mitatu baadaye, wasimamizi wa ndoa walimtaka arudi Dar kwa ajili ya kujua hatima ya ndoa yake.
Aliambatana na kaka yake hadi nyumbani kwa mumewe, cha ajabu walimkuta hausigeli akiwa na mtoto mchanga. Aliwazuia kuingia ndani akidai hawakuwa na mamlaka hayo.
Alisema kaka yake alimtaka hausigeli ampigie simu mchungaji amwambie shemeji yake anamhitaji, alifanya hivyo na mchungaji alifika lakini alipowaona alitoka nduki.

WAZEE WA KANISA WAINGILIA KATI
Aliendelea kudai kuwa ulifika wakati wazee wa kanisa waliingilia kati, wakamuweka mchungaji kikao na kumuuliza kulikoni hawamuoni mke nyumbani badala yake msichana wa kazi tena akiwa na kichanga.
“Cha kushangaza mchungaji alipandwa na hasira, akawafanyia fujo wazee hao, alimpiga na kiti mzee mmoja ambaye alikuwa msaidizi wake anayeitwa Kisaka na kumjeruhi,” alisema mama mchungaji.
Alisema sakata la kujeruhiwa kwa Kisaka liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Mbezi Kwayusuf na kufunguliwa jalada namba KMR/RB/2125/2013- SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI.

AVULIWA UCHUNGAJI
Alisema katika kikao hicho, wazee hao walifikia uamuzi wa kumvua rasmi uchungaji kwa kumwandikia barua na kumkabidhi.
Mchungaji aliipokea barua hiyo lakini hadi sasa anaendelea na huduma kwani wapo waumini wachache walio upande wake huku wengine wakidaiwa kulikimbia kanisa hilo.

BOFYA HAPA UMSIKIE MCHUNGAJI
Baada ya kuzinyaka habari hizo, Juni 18, mwaka huu, mapaparazi wetu walimtafuta Mchungaji Mariki na kufanikiwa kumkuta nyumbani kwake Kimara-Mwisho ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Siwezi kuzungumzia lolote kuhusu habari alizosema mke wangu kwa sababu suala hili lipo kwenye Baraza la Usuluhishi wa Ndoa na lipo kwa maandishi, naweza kuwaambia kuwa kuna watu wanataka kunipindua, wanapanga hila na njama ili walichukue kanisa na ndiyo wanamtumia mke wangu lakini hawawezi, wameshindwa.
“Kuhusu kuzaa na hausigeli wangu ni kweli na mtoto ana miezi saba sasa, lakini hizo shutuma kwamba alikuwa na miaka 15 siyo kweli, alikuwa na miaka 17 na sasa ana miaka hiyohiyo.”

HAUSIGELI VIPI?
Risasi Jumamosi lilizungumza pia na hausigeli ambaye anaishi na mchungaji huyo kwa sasa kama mke ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Anayesema nilikuwa na miaka 15 ana ushahidi? Wanaoweza kujua umri wangu ni wazazi wangu na ukweli ni kwamba mwezi wa kumi mwaka huu natimiza miaka kumi na nane.
“Kuhusu kwamba nilikuja kufanya nini Dar, nilikuja kwa mume wangu mwenye ushahidi kuwa nilimfukukuza mke wake alipokuja nyumbani aniletee.”
Hata hivyo, Risasi Jumamosi linaendelea kufuatilia sakata hili ili kukujuza nini hatima yake.

Share:

MIMBA YA PENNY YACHOROPOKA..... PENZI LAKE NA DIAMOND LAKAA PABAYA...!!!


TAARIFA ya ndani zinazodai kwamba, mimba ya mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nassibu Abdul ‘Diamond’, Peniel Mgilwa ‘Penny’ imechoropoka zimevujaKwa mujibu wa chanzo makini kilichojitambulisha kwa jina la wifi (jina kapuni) kwa Penny, ni kwamba mtangazaji huyo wa Runinga ya Channel 10 cha jijini Dar hivi sasa hana ujauzito tena kama wengi wanavyodhani.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo, wifi huyo alisema kwamba awali kulikuwa na dalili zilizoonesha kwamba Penny alikuwa ni mjamzito kutokana na mtangazaji huyo kutumia vitu vichachu kama vile maembe na mara kwa mara alikuwa akiumwa hadi kufikia kulazwa hospitali.
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Mwandishi: Mambo vipi, Penny pole sana.
Penny: Pole ya nini sasa?
Mwandishi: Si nimesikia kwamba unaumwa jamani na ukakumbwa na mkasa mwingine?
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Mwandishi: Nilisikia kwamba baada ya kuumwa na kulazwa hopsitali mimba yako ikatoka?
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Mwandishi: Sasa unatarajia lini utapata tena mimba nyingine?
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa.

Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive