Tuesday, 21 April 2015

Waziri wa TAMISEMI ameitaka mifuko ya jamii kusaidia watumishi kupata makazi.

Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu serikali za mitaa na tawala za mikoa TAMISEMI Mh. Hawa Ghasia ameitaka mifuko ya hifadhi ya jamii nchini isaidie watumishi kupata makazi hasa sekta ya afya ili waweze kutoa huduma bora na kwa wakati muafaka.
Mh Ghasia ametoa wito huo jijini dar es salaam wakati wa utiliaji saini makubaliano kati ya shirika la elimu kibaha na watumishi HOUSING kuhusu mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma zinazotarajiwa kujengwa ndani ya eneo la shirika hilo ambapo amewataka kulenga maeneo yenye upungufu mkubwa wa nyumba za watumishi.
 
Kwa upande wake mkurugenzi wa NHC Dk. Fred Msemwa amesema kupitia ubia huo katika kipindi cha miaka mitano watajenga nyumba 1,150 pamoja na miundombinu mingine inayoendana na huduma za jamii na hivyo kutawawezesha wafanyakazi mbalimbali waliopo ndani na nje ya kibaha kunufaika na kuongeza kuwa nyumba hizo watauziwa watumishi wa umma na baadae wananchi wa kawaida kwa masharti nafuu.
Share:

Serikali ya Tanzania imesema hakuna watanzania waliouawa katika matukio ya mauji Afrika kusini.


Serikali imesema hakuna mtanzania aliyeuawa katika matukio ya mauji ya  chuki za kibaguzi (ZENOPHOBIA) yanayofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya wageni na tayari imeanza mpango wa kuwarudisha nyumbani watanzania 21 kati ya 23 waliohifadhiwa katika kambi kwenye mjini DURBUN nchni humo kwa ajili ya usalama.
Akizungumza na waandishi wa habari waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mhe. Bernad Membe amesema  vifo vya watanzania watatu vilivyotokea nchni humo havina mahusiano na mauaji hayo ZENOPHOBIA na kusisitiza serikali ya afrika kusini imeanza kuchukua hatua na tayari watu wawatu waliohusika na kifo cha rais wa msumbiji wamekamatwa.
 
Akizungumzia idadi ya watanzania waliohifadhiwa kwenye 
Kambi katika mji wa DURBUN,Mhe Membe amesema takribani watanzania 23 wamehifadhiwa katika kambi ya isipingo iliyo  na zaidi ya raia  wa kigeni elfu tatu ambao wako chini ya ulinzi wa serikali ya afrika kusini na kusisitiza serikali imeanza utaratibu wa kuwarudisha nyumbani watanzania 21 kati yao.
 
Akielezea msimamo wa tanzania kufuatia mauaji hayo ya ZENOPHOBIA yanayoendelea nchni afrika kusini,Mhe. Membe amesema serikali inaunga na jumuiya ya nchi za SADC kulaani vitendo vya mauaji yanayoendelea nchni humo ambapo watu 8 wamekwisha uawa kikatili na kuita serikali ya afrika kusini kuzuia mauaji hayo haraka iwezekanavyo.
 
Aidha amesema serikali ya Tanzania haitakuwa na tatizo la watanzania kurudi nchni humo baada ya mauaji kudhibitiwa na kwa upande wa wafanyabishara walisajiliwa kihalali na kupoteza mali zao, serikali itawasiliana na wanasheria wake ili kuona namna ya kutafuta namna ya nchi hiyo kuwafidia hasara waliyoipata.
Share:

Serikali yatakiwa kuvishirikisha vikundi vya uhamasishaji kukabiliana na mauaji ya imani za kishirikina.

Vikundi vya vijana vinavyotumika kuhamasisha jamii kwenye majukwaa ya kisiasa vikijengewa uwezo vina uwezo mkubwa wa  kusaidia kuelimisha jamii kuondokana na imani za  kishirikina ambazo licha ya kuwa kikwazo cha maendeleo zimekuwa chanzo kikubwa cha umwagaji wa damu .
Akizungumza katika ibada maalumu ya kuhamasisha jamii kujiepusha na vitendo vya kishirikina iliyoanadaliwa na wadau mbali mbali kwa ushirikiano na kanisa la Pentekost   kamanda wa vijana wa mkoa  wa Arusha Bw. Philemon Molllel amesema baada ya kubainika kuwa ushirikina ndio msingi mkuu wa mauaji ya walemavu wa ngozi,vikongwe,na maovu mengine  katika jamii kinachohitajika ni kushirikiana na kuhamasishana kuutokomeza kazi  ambayo  vikundi hivyo vinaiweza.
 
Baadhi ya washiriki wa hafla hiyo wakiwemo wanaounda vikundi vya uhamasishaji wamesema  wakiwezeshwa na kushirikishwa kupunguza vitendo hivyo ni jambo linalowezekana kwani yote hayo ni matokeo ya mmomonyoko wa maadili tatizo ambalo ufumbuzi wake ni kuelimisha jami
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive