Sunday, 16 June 2013

MTWARA-BIBI KIZEE ALIYESEMA ATAGEUZA GESI KUWA MAJI ATOWEKA



KIKONGWE Somoe Issa, anayekadiriwa kuwa na umri zaidi ya miaka 90, ambaye aliwahi kutishia kuigeuza gesi kuwa maji iwapo serikali itaendelea kulazimisha kusafirisha kwenda Dar es Salaam, sasa hajulikani alipo.

Taarifa zilizoifikia MTANZANIA Jumapili ambayo ipo mkoani Mtwara, zilidai kuwa bibi huyo baada ya kutoa tishio hilo sasa amefichwa, ili asiweze kutekeleza lengo lake hilo.

Bibi Somoe, anayeaminika kama Mkuu wa Kaya ya Msimbati, kijiji ambacho gesi asilia iligundulika, sasa hajulikani alipo, huku ndani ya kijiji hicho ulinzi mkali ukiwa umeendelea kutawala.

Ulinzi umeimarishwa katika kijiji hicho, lengo likiwa ni kuhakikisha hakuna mtu anayefika karibu na nyumba aliyokuwa akiishi bibi huyo.

MTANZANIA Jumapili, lilifika katika kijiji hicho juzi, ambako liliweza kuzungumza na Mwenyekiti wa Kijiji cha Msimbati, Salum Athuman Tostao, ambaye alikiri kuwa bibi huyo hayupo na wala haifahamiki alikopelekwa.

“Ni kweli bibi huyu hajaonekana tangu palipotokea vurugu na watu wa usalama waliokuwa wakitaka kumuiba, kama unavyofahamu kulikuwa na mtu aliyejifanya mwandishi wa habari alitaka kumuiba bibi huyu, lakini wanakijiji wakamshtukia na kuchoma gari lake moto.

“Kutokana na hali hiyo, mpaka sasa hatufahamu alipo na hatujui kama ni serikali au wanafamilia wamemficha, kwa sababu kwanza hawaturuhusu hata sisi ambao ni viongozi kufika maeneo ya nyumba aliyokuwa akiishi kwa sababu wanadhani tutaleta watu wengine wasiokuwa waaminifu kwa familia hiyo,” alisema Tostao.

Gazeti hili lilipomtafuta mtoto wa bibi huyo, Manzi Faki, alikataa kuzungumza chochote kuhusu mama yake, lakini aliitaka serikali kutekeleza ahadi zake kwa Wanamtwara.

“Hilo suala la mama sitaki kulizungumzia kabisa… jambo la muhimu serikali inapaswa kufahamu kuwa sisi wana Mtwara tunataka itekeleze ahadi ilizotuahidi ndipo waje kuchukua hicho kidogo wanachokitaka, zaidi ya hapo kijumla gesi haitoki,” alisema Faki.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtandi, Salum Waziri, alieleza kuwa bibi huyo anaaminiwa na wanakijiji wenzake kutokana na uwezo wake wa kuzuia mambo yasiyotakiwa ndani ya jamii, sambamba na kuleta riziki pale wanapokwenda kumuomba.

“Kwa kweli sasa ulinzi mkali umeimarishwa na wanakijiji, hakuna mtu anayefika nyumbani kwake, hata sisi wenyewe hatuthubutu, ndiyo maana hatufahamu alikopelekwa.

“Nakumbuka bibi aliwahi kutumiwa na kampuni ya Artumas kukwamua mashine iliyokuwa imenasa katika mchakato wa uchimbaji wa gesi hiyo baharini, ambapo wazungu hao walihangaika kuita wahandishi nje ya nchi, lakini wote wakashindwa, ndipo waliponong’onezwa kuhusu bibi huyo wakamwendea na akaja kunasua.

“Wakampa zawadi ya kumjengea nyumba, haya ni mambo ambayo yalitokea mwaka 1994, kiujumla yapo mengi ambayo yametufanya tumwamini sana,” alisema Waziri.

Januari mwaka huu, Afisa usalama mmoja anayedaiwa kufahamika kwa jina la babu alijikuta katika wakati mgumu kiasi cha gari lake kuchomwa moto huku yeye mwenyewe akikimbilia kusikojulikana baada ya kuzuka vurugu kubwa wakati akimshawishi bibi huyo asizuie gesi kwenda Dar es salaam.

Inadaiwa kuwa mwanausalama huyo alitumwa na viongozi wa juu wa serikali baada ya bibi huyo kutamka wazi kuwa gesi haitoki Mtwara kauli ambayo iliwafanya viongozi kupata wasiwasi na hivyo kumtuma mtu huyo ili amshawishi bibi huyo.

Wakati bibi huyo akizungumza na mwanausalama huyo inadaiwa kuwa aliwaita wajukuu zake wamsikilize ndipo vurugu kubwa zilipoibuka na kusababisha mwanausalama huyo atimue mbio huku akilitelekeza gari lake.

Juzi na jana baadhi ya wakazi wa kijiji hicho wakizungumza na gazeti hili walisema wao hawazuii gesi kutumiwa na Watanzania, ila wanataka gesi hiyo ichakatwe hapohapo mkoani Mtwara na ndipo isafirishwe kuelekea sehemu nyingine.

Vurugu kuhusu gesi hii ya Mtwara zilianza kuibuka Novemba mwaka jana, wananchi wa mkoa huo walikuwa wakipinga ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam.

Pamoja na vurugu hizo kuzimwa mara kadhaa na Jeshi la Polisi, ambao sasa wanashirikiana na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), lakini bado MTANZANIA Jumapili imeshuhudia hali ya amani haijaweza kurejea mkoani humo.

Baadhi ya watu mkoani hapa, bado wanaendeleza visasi kwa kuchoma nyumba za wenzao, huku JWTZ wakidaiwa kuwapiga raia kila mara hata inapotokea kuwa wamezomewa.
TOA MAONI YAKO HAPA
Share:

UKWELI WA MAMBO KUHUSU MAMA ALIYEAMUA KUISHI UCHI JUU YA PAA LA NYUMBA HUKO MBEZI BEACH


WIKI iliyopita kuliibuka sakata zito lililochukua nafasi kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, lililomuhusisha mama mmoja aliyejulikana kwa jina la Hezelina Mrema mkazi wa Mbezi Beach, eneo la Tangi Bovu jijini Dar es Salaam, kuamua kuishi juu ya paa la iliyodaiwa kuwa ni nyumba yake.
Hatua hiyo ilisababisha baadhi ya wanaharakati kujitokeza na kuahidi kumsaidia mama huyo, aliyedai kuwa anataka kutolewa kwa nguvu ndani ya nyumba yake halali, ambayo ameijenga na mumewe Samwel Opulukwa.

UKWELI WA MAMBO

Ukweli juu ya suala hilo ni kwamba Hezelina hahusiki kwa namna yeyote na nyumba hiyo, ambayo ni ghorofa moja, kwani imebainika kuwa si mke halali wa Opulukwa na badala yake wana mahusiano ya kimapenzi.
Imebainika kuwa mke halali wa Opurukwa alisha achana nae na mke wake huyo tayari alishaweka pingamizi Mahakamani la kutaka hati ya nyumba hiyo isibadilishwe mmiliki.
Mbali ya Hazelina kutokuwa mke halali wa Opulukwa pia imebainika kwamba mwanaume huyo aliitumia nyumba hiyo kuweka dhamana ya mkopo kwenye benki ya TIB.

Imebainika kuwa hatua ya Opulukwa kuweka nyumba yake dhamana ilikuja baada ya rafiki yake ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Asasu Express Ltd kuhitaji fedha za kuendeshea bishara yake, lakini alikumbana na kikwazo cha kutakiwa kuwa na nyumba jijini Dar es Salaam, ambapo kwa kuwa hakuwa nayo aliona amtumie rafiki yake huyo kufanikisha mkopo wake kwa makubaliano kuwa ataulipa bila tatizo.

Hata hivyo mmiliki huyo wa kampuni ya Asasu alishindwa kulipa mkopo huo wa mamilioni ya fedha, ambapo benki husika ilianza harakati za kutaifisha mali zake ili kufidia deni hilo, hata hivyo hazikutosha na ndipo walipoamua kuiuza nyumba hiyo ya Mbezi Beach iliyopo kiwanja namba 235 Block D.

Imeelezwa kuwa benki ya TIB ilimpa Opulukwa taarifa zote za deni husika pamoja na kumpa Notisi ya kumtaka alipe deni husika ambalo ni 274,854, 256. 84 kutokana na rafiki yake kushindwa kulipa deni husika pamoja na mali zake kutaifishwa.

Ili kufuata taratibu za kisheria za kutaifisha nyumba ya Opulukwa, benki hiyo ilitoa tangazo la kutoa tenda ya kuuza nyumba hiyo, ambalo lilitolewa kwenye gazeti la serikali Januari 10,2011.
Hata hivyo Opulukwa hakutoa ushirikiano wowote, hali iliyosababisha benki ya TIB kuipiga mnada nyumba hiyo na kufanikiwa kupata mteja, ambaye aliinunua kihalali ikiwa ni pamoja na kubadilisha hati miliki ya nyumba hiyo.
Jambo la kushangaza Opulukwa aliendelea kuishi ndani ya nyumba hiyo, TIB ilifanya harakati za kumtoa kwa kuyatumia makampuni kadhaa ya udalali ambayo yalishindwa kufanikisha kazi hiyo na ndipo Machi mwaka huu, jukumu hilo la kumtoa Opulukwa lilipelekwa kwa kampuni ya udalali ya Msama Auction Mart.

Baada ya Kampuni ya Msama Auction Mart kufanya taratibu zake za kikazi na kuridhishwa na uwepo wa deni husika, Juni 8, mwaka huu ilifika eneo la tukio na kuanza kumtoa Opulukwa.

Hata hivyo zoezi hilo lilikuwa gumu kutokana na baadhi ya maofisa wa Polisi wa Wilaya ya Kinondoni kuingilia kati, ambapo waliitisha kikao cha pamoja kati ya maofisa wa kampuni ya Msama Auction Mart na Opulukwa, ambapo maamuzi yalikuwa ni kusimamisha zoezi hilo hadi pale mkopaji huyo atakapopata baraka za Mahakama juu ya uhalali wa kuendelea kuishi kwenye nyumba hiyo.
Baada ya maamuzi hayo ya jeshi la polisi, Opulukwa alifungua kesi ya madai ya kuvunjiwa nyumba yake na kuibiwa vifaa vyenye thamani ya shiringi 195 milioni, jambo ambalo halikuwa na ukweli wowote.

Juni 11, mwaka huu mara baada ya Opulukwa kukosa vielelezo vilivyompa uhalali wa kuendelea kuishi ndani ya nyumba hiyo kama alivyoagizwa na Mkuu wa Polisi wilaya Kinondoni, kampuni ya Msama Auction Mart iliendelea na zoezi la kumuondoa.

Wakati maofisa wa kampuni ya Msama Auction Mart wakiwa na uhakika wa kukamilisha zoezi lao pamoja na kuondoka eneo hilo,ghafla walipigiwa simu na walinzi walioachwa kwenye eneo hilo kuwa kuna mtu yupo ndani ya nyumba, ambaye inaelezwa aliruka ukuta ili kufanikisha lengo lake.

Hatua hiyo ya Hazelina iliwashangaza maofisa wa Msama Auction Mart, ambao walichukua jukumu la kupiga simu polisi ili kuhakikisha mama huyo anaondolewa kwa njia ya amani na utulivu.
Wakati huo tayari Hazelina alikuwa ameshapanda juu ya paa la nyumba hiyo, huku akitishia kujirusha ili kuutoa uhai wake endapo angetolewa kwa nguvu.

Aidha alikwenda mbali zaidi kwa kuvua nguo ili kuonesha utupu wake, lengo lake likiwa ni kutowapa nafasi walinzi wa kiume kutomsogelea.

Hatua ya mama huyu kuonesha utupu wake na kuendelea kukaa juu ya paa la nyumba hiyo ilizua maswali na kuwafanya baadhi ya waandishi wa Habari kufika eneo hilo ili kujua ukweli wa mambo.

Kutokana na kauli za uongo za mama huyo, alifanikisha kuwaaminisha waandishi wa habari kuwa kuna hila zinafanyika ili kupora nyumba yake, ambayo alidai kuwa ni halali yao.
Hata hivyo maamuzi ya mama huyo kuendelea kukaa juu ya paa la nyumba hiyo, yalidumu kwa muda wa siku mbili, ambapo Juni 13, mchana kwa hiyari yake aliamua kushuka baada ya kumuona jamaa yake akiwa ameshikilia karatasi zilizodaiwa kuwa zimetoka Mahakama ya Kinondoni.
Uchunguzi wa wetu umebaini kuwa Opulukwa hakumueleza ukweli mama huyo, ambapo ukweli halisi wa zoezi zima la kuhamishwa kwenye nyumba hiyo analijua.

Aidha imebainika kuwa mwanamama huyo si mke wa Opulukwa, kwani mke wake halali anajulikana kwa jina la Rachel Paulo Ng’wahi, amabaye ndiye aliyefungua kesi ya kupinga hatua ya mume wake kutumia nyumba yao kumuwekea dhamana ya mkopo rafiki yake ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Asasu.

Ukweli ni kwamba benki ya TIB na kampuni ya Msama Auction Mart, walikuwa sahihi kumuondoa Opulukwa kwenye nyumba hiyo, hakuna sheria yeyote waliyoivunja na hawakuwa na nia ovu ya kutaka kumpora mama huyo na Opulukwa aliyedai kuwa ni mumewe nyumba kama alivyodai kwenye vyombo vya habari
Share:

KIM KARDASHIAN AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE...!!!

NI siku ya furaha kwa Kanye West! Kim Kardashian amejifungua mtoto wa kike Jumamosi asubuhi katika hospitali ya Cedars-Sinai Medical Center, Los Angeles, mtandao wa OMG umethibitisha.

Inasemekana Kardashian, 32, alikuwa na West pembeni mwake wakati wa kujifungua, kumkaribisha duniani binti yao mwezi mmoja kabla ya muda uliotarajiwa. Tarehe halisi ya kujifungua ilitazamiwa kuwa Julai 11.

"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye kupata mtoto mapema," chanzo cha hospitali kimeileza Us Weekly. “Inafurahisha, wote katika hali nzuri!"

Kanye West, 36, na Kim - wote wawili wakiwa ndo mara ya kwanza kuwa wazazi, wamekuwa wapenzi tangu Aprili 2012. Desemba 30, 2012, West alitangaza kwamba mpenzi wake alikuwa na mimba wakati wa tamasha lake Atlantic City.

"Simamisha muziki na wote mpige kelele kwa mama kijacho," alisema West jukwaani akionyesha kidole kwa Kim ambaye alikuwa mmoja wa watazamaji.

Share:

OMMY DIMPOZ AANZA SAFARI YA KWENDA NYUMBANI KWA AKINA MANGWEA KUOMBA MSAMAHA


Kutokana na kauli aliyotoa msanii Ommy Dimpoz ya SITAKUFA KIJINGA NA KIMASIKI KAMA KAMA ALIVYOKUFA NGWAIR, hii ndio kauli aliyotoa baada ya mashabiki na Wanamuziki wenzake kumaind kwa kile
NANUKUU:
"Samahani tena sana sitawacha kuomba msamaha, nimekubali makosa na hivi sasa naelekea nyumbani kwao kuomba msamaha kwa familia na nitue kwa vituo vya radio kuomba msamaha kwa wabongo na wote niliowaudhi. Samahani sana na nakubali mimi si mtu bila nyinyi na sikuongea kuhusu legend Ngwair kwa ila mbaya. One love". mwisho wa kunukuu
Share:

BINTI ACHOMWA MOTO HADI KUFA BAADA YA KUOMBA AOLEWE NA NDUGU YAKE...!!!

Msichana wa miaka 19 amechomwa moto hadi kufa na mama yake kupigwa baada ya kuwaomba wazee wa kijiji kuruhusiwa kuolewa na mvulana mmoja kutoka kijijini hapo na ukoo mmoja, polisi wa India wamethibitisha.
Anju Yadav, kutoka kijiji cha Karahkol, wilayani Deoria katika jimbo la Uttar Pradesh, alichomwa moto nyumbani kwake wakati mama yake, Gyanwati Devi, mwenye miaka 48, alipokuwa upande mwingine wa kijiji hicho akiiomba halmashauri ya kijiji kumruhusu Anju aolewe na rafiki yake wa kiume aliyekuwa na mahusiano naye kwa miaka miwili, Ranjit Yadav, mwenye miaka 21.
Lakini halmashauri ya kijiji hicho, sambamba na baba wa mvulana huyo, Jai Hind Yadav, mwenye miaka 52, walitupilia mbali maombi hayo wakisisitiza ilikuwa kinyume cha utamaduni.

Badala yake, baba wa mvulana huyo alikimbilia kwenye nyumba ya familia na kumchoma moto msichana huyo, ilidaiwa.
Jamii ya India inafahamika mno kwa mfumo wake wa ukoo ulioingiliana, ambao unaweza kuzuia watu kutoka jamii tofauti kuoana na katika baadhi ya matukio kuafikiana na jambo kama hilo.

Hatahivyo, inaeleweka kwamba haikubaliki kwa watu kutoka ukoo mmoja na kijiji kuoana. Ndoa ndani ya Gotra (ukoo) mmoja pia hairuhusiwi katika utamaduni wa India, hasa katika mikoa ya kaskazini mwa nchi hiyo ambako makundi ya kiukoo, yanayofahamika kama Khap Panchayats, yanachukulia ndoa kama hizo kuwa kosa la jinai.


Rakesh Kumar, mkuu wa Kituo cha Polisi cha Ikauna, alisema: "Jai Hind pamoja na wanakijiji wengine watatu walikimbilia nyumbani kwa msichana huyo na kumwagia mafuta na kisha kuchoma moto wakati mama yake akiwa kwenye kikao hicho cha halmashauri. Tumewakamata wafuasi wawili wa kundi hilo wakati wengine wawili wakiwa wanaendelea kusakwa."
Anju aliungua asilimia 85 ya mwili wake wote na alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa hospitali Alhamisi jioni.


Anju alikuwa peke yake wakati wanaume hao wanne walipovamia nyumbani kwake. Katika kuchanganyikiwa aliruka kutoka kibarazani kwake hadi ghorofa ya pili kujaribu kujiokoa. Alivunjika mikono na miguu yake.


Wanakijiji walimmwagia maji, lakini wakati huo alikuwa tayari amepata majeraha makubwa ya moto.
Mama yake, Gyanwati, alisema wote binti yake na Ranjit walipendana sana na kudhamiria kufunga ndoa.


Gyanwati alikwenda nyumbani kwa Jai Hind Jumatano jioni kujadiliana kuhusu suala la ndoa lakini pale yeye na familia hiyo walipokataa alikwenda katika baraza la kijiji kwa msaada, jambo la kawaida katika India.


Gyanwati alisema: "Nilitaka kumwona binti yangu akiwa mwenye furaha. Walipendana mno; sikuwa na tatizo na ndoa yao. Lakini pale nilipokwenda kwa Jai Hind na maombi hayo alinieleza ni dhambi kuoana ndani ya ukoo mmoja na hatokubaliana na ndoa hiyo."
Polisi wamethibitisha kwamba Jai Hind bado hajapatikana.
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive