Mh Ghasia ametoa wito huo jijini dar es salaam wakati wa utiliaji
saini makubaliano kati ya shirika la elimu kibaha na watumishi HOUSING
kuhusu mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma zinazotarajiwa
kujengwa ndani ya eneo la shirika hilo ambapo amewataka kulenga maeneo
yenye upungufu mkubwa wa nyumba za watumishi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa NHC Dk. Fred Msemwa amesema kupitia
ubia huo katika kipindi cha miaka mitano watajenga nyumba 1,150 pamoja
na miundombinu mingine inayoendana na huduma za jamii na hivyo
kutawawezesha wafanyakazi mbalimbali waliopo ndani na nje ya kibaha
kunufaika na kuongeza kuwa nyumba hizo watauziwa watumishi wa umma na
baadae wananchi wa kawaida kwa masharti nafuu.





