Monday, 8 July 2013

Matonya bado ahaha rumande Songea

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Seif Shaban maarufu kama Matonya 

Dar. Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Seif Shaban maarufu kama Matonya bado anaendelea kusota rumande mjini Songea baada ya kukataliwa dhamana kutokana na kufanya utapeli baada ya kulewa kupita kiasi na kushindwa kufanya shoo iliyoandaliwa na promota mmoja mjini humo.

Matonya alitakiwa kufanya shoo kwenye Ukumbi wa Jambolee uliyopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Matonya alifika ukumbini akiwa amelewa hali iliyompelekea kushindwa kufanya show na kusababisha hasara katika ukumbi baada ya kufanya fujo ya kuvunja vitu ukumbi hapo, Ndipo waandaaji wa show hiyo walipoamua ifanyike kesho yake na kiingilio kiwe ni kununua bia .

Wakati huo msanii huyo alitakiwa akafanye show nyingine Wilaya ya Mbinga ambayo ilikuwa ni sehemu ya mkataba wao lakini hakufanya hivyo na matokeo yake akaamua kukata tiketi kurudi Dar es Salaam. Baada ya kuvuja taarifa hizo walimfata hadi alipokuwa amefikia na kukuta amehamia sehemu nyingine.

Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive