Monday, 20 April 2015

LHRC yaitaka serikali kutoa machapisho ya kutosha ya katiba pendekezwa.

Wakati taifa likielekea kuipigia kura katiba inayopendekezwa kumejitokeza changamoto  ya upatikanaji wa  katiba hiyo kutokana na kuwepo na machapisho machache ya katiba inayopendekezwa na hivyo kituo cha sheria na haki za binadamu(LHRC) kimeitaka serikali kuchapisha  machapisho ya kutosha ya katiba hiyo ili wananchi waweze kuisoma na kuielewa.
Hayo yameelezwa na mwanasheria wa kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) Bi.Geline Fuko wakati akizungumza katika mikutano mbalimbali ya kutoa elimu kuhusiana na katiba inayopendekezwa  mjini songea.
 
Bi.Geline Fuko amesema katika maeneo mbalimbali waliyozunguka wamebaini kuwa  machapisho ya katiba  pendekezwa  yako machache hivyo wameitaka serikali  kuchapisha machapisho hayo ya kutosha.
 
Katika mkutano uliofanyika chuo cha ualimu Songea TTC na kuwashirikisha wanachuo na walimu katika chuo hicho wanachuo wamekosoa katiba pendekezwa  kutokidhi matakwa ya wananchi.
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive