Wakizungumza na ITV katika ofisi za Chadema kanda ya magharibi
mjini Tabora, viongozi wa Bavicha na Chaso, wameonesha wasiwasi mkubwa
wa kudai kuanza kwa mizengwe ya kunyimwa haki ya kupiga kura kutokana na
mkanganyiko katika fomu ya maombi ya utambulisho wa mpiga kura
inayotolewa na tume ya taifa ya uchaguzi wanazotakiwa kujaza na
wanavyuo, na utaratibu mzima wa zoezi la uchaguzi litavyoendeshwa
wakilinganisha na lile la uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 hasa kwa kufungwa
vyuo na wanafunzi kurudi makwao maeneo ambayo kimsingi
hawakujiandikishia katika daftari la kudumu la mpiga kura.
Katibu wa Chadema mkoa wa Tabora Bw.Alinanuswe Edson ameiomba
serikali kulishughulukia mapema suala hilo ambalo amedai huenda likaleta
mzozo ambao pengine ukasababisha athari kubwa hususani kwa vijana.
Aidha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 baadhi ya wanafunzi wa
vyuo imedaiwa kuwa hawakupata fursa ya kupiga kura ipasavyo kutokana
na kuwepo kwa mkanganyiko uliosababishwa na kuondoka maeneo ambayo
walijiandikishia kupiga kura na hivyo kuleta usumbufu mkubwa katika
kuteleza haki hiyo ya kimsingi.





