Monday, 22 June 2015

KCEE ANASWA SOKONI AKINUNUA MAFUTA YA MAWESE

STAA wa 'Limpopo', Kcee akiwa kwenye soko kuukuu akinunua mafuta ya mawese pamoja na matunda.
LAGOS, Nigeria
STAA wa 'Limpopo', Kcee wikiendi iliyopita alituma picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa sokoni.
 Kcee siyo mgeni kwa wadau wa muziki wa Bongo, kwani ameshafanya ngoma na Shetta inayoitwa Shikorobo lakini pia amemshirikisha Diamond Platinumz  katika wimbo mpya wa ‘Love Boat’.
 Kcee alituma picha hiyo akionekana akiwa kwenye soko kuukuu akinunua mafuta ya mawese pamoja na matunda huku baadhi ya wauzaji na wanunuzi waliokuwepo eneo hilo wakimshangaa.
Baada ya kupost picha hiyo, mashabiki waliofanikiwa kuiona walimpongeza kwani ni ngumu sana kwa msanii kuonekana akiwa kwenye soko ‘lililochoka’ akinunua vitu.
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive