LAGOS, Nigeria
STAA wa 'Limpopo', Kcee wikiendi iliyopita alituma picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa sokoni.
Kcee siyo mgeni kwa wadau wa muziki wa Bongo, kwani ameshafanya ngoma na Shetta inayoitwa Shikorobo lakini pia amemshirikisha Diamond Platinumz katika wimbo mpya wa ‘Love Boat’.
Kcee alituma picha hiyo akionekana akiwa kwenye soko kuukuu akinunua mafuta ya mawese pamoja na matunda huku baadhi ya wauzaji na wanunuzi waliokuwepo eneo hilo wakimshangaa.





