Sunday, 2 June 2013

Maelfu waandamana Addis Ababa

                                           Maelfu ya waandamanaji wameandamana katika barabara za mjini Addis Ababa, Ethiopia, wakidai waandishi wa habari na wanaharakati walioko kizuizini wafunguliwe.
                              Waandishi wa habari wanasema ni nadra kuonesha upinzani wa namna hiyo kwa chama tawala ambacho kinadhibiti shughuli za jamii sawasawa.

Makundi ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema serikali imetumia sheria za kupambana na ugaidi ili kuwafunga waandishi wa habari.

Waandamanaji- wengi kutoka upinzani - walipiga kelele kudai uhuru na haki.

Haya ni maandamano ya kwanza tangu mwaka wa 2005 ambapo mamia ya waandamanaji waliuliwa katika ghasia zilizofuatia uchaguzi.

















Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive