Thursday, 8 August 2013

FEZA : Ana bendera tatu mkononi

feza kessy

MCHEZO wa kutoana na nani ataibuka mshindi umekuwa wa kikanda zaidi au ukaribu wa mipaka ya nchi, kuanzia jinsi washiriki wanavyopendekezana na hata Afrika inavyopiga kura katika shindano la Big Brother Africa (BBA).

Kwa wiki tatu mfululizo tumeshuhudia mshiriki wa Kenya akipata kura tatu kila wiki nazo ni za Tanzania, Uganda na Kenya yenyewe.

Washiriki wanaowakilisha nchi za Afrika Magharibi wamekuwa wakiwapendekeza washiriki wa Mashariki au Kusini mwa Afrika.

Mshiriki anayeiwakilisha Tanzania na pengine sasa Afrika Mashariki, Feza Kessy, kesho Jumapili ana mtihani mgumu wa kuiinua Afrika Mashariki kwani ili abaki anahitaji kura kutoka nchi zisizopungua tano.

Katika kikaango yupo na mshiriki kutoka Botswana, Oneal na Bimp kutoka Ethiopia. Kutokana na upigaji kura unaoangalia kanda, Feza angejihakikishia kura ya Ethiopia na ya nchi nyingine zisizo na washiriki.

Kura za uhakika ambazo anazo mkononi mpaka sasa ni ya Kenya, Uganda na Tanzania. Kura ya Ethiopia ameikosa kwa kuwa wanaye mshiriki wao katika kitanzi, Bimp.

Nchi kama Ghana ziliwahi kumpigia kura Feza, lakini mchezo umebadilika na kuna malumbano kati ya Elikem ambaye ni mwakilishi kutoka nchi hiyo.

Kura ya Botswana pia ataikosa kwa kuwa ‘shemeji’, Oneal kutoka nchi hiyo naye yupo kwenye kikaango akitegemea huruma za Afrika ili aweze kubakia katika mashindano hayo.


Washiriki wa Afrika Mashariki

Washiriki kutoka Kenya ni Huddah na Uganda ni Denzel, hao walikuwa wa kwanza kuyaaga mashindano hayo katika wiki ya kwanza.

LK4 kutoka Uganda naye alifuatia wiki moja baadaye na kuwaacha Annabel kutoka Kenya, Nando na Feza kutoka Tanzania wakiwakilisha.

Annabel kwa kutumia kura za nchi tatu yaani Kenya, Uganda na Tanzania, alipona katika kikaango mara nne mfululizo kabla ya kutolewa wiki iliyopita.

Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive