MSANII wa muziki wa kizazi kipya, King Kapita, ameachia ngoma mpya inayokwenda kwa jina la ‘Kasema Poa’.
Kwa mujibu wa King Kapita, kazi hiyo imeandaliwa katika studio mbili kubwa nchini Nigeria na Tanzania, hivyo anaamini itawashika vilivyo mashabiki kutokana na ubora wake.
King Kapita alisema katika ngoma hiyo amewashirikisha pia Wanigeria, DJ maarufu aitwaye Kalito na DJ Ryder.
King Kapita katika moja ya mashairi ya ngona hiyo anasema: “Sasa tunaimba na kucheza wote, kamwambieni yule mtoto mzuri kasema poa, yanii she say yeahhhh...”
Ngoma nyingine zinazobamba za msanii huyo mmoja wa waasisi wa kundi la Wakacha, ingawa sasa anajitegemea ‘Solo artist’ ni pamoja na ‘Shikamoo Pesa’, ‘Kuna tatizo Kwani’ na sasa kaachia ‘Kasema Poa’.
Msanii huyo aliongeza kuwa, hivi sasa ngoma hiyo inapatikana mtandaoni na kuomba sapoti kutoka kwa wadau mbalimbali wa sanaa.






