Sunday, 11 August 2013

Neville ataka United isimuuze Rooney


MANCHESTER, ENGLAND

JAMANI acheni! Acheni kabisa. Ndivyo ambavyo beki wa zamani wa Manchester United, Gary Neville, ameisihi klabu yake hiyo kuachana na mpango wa kumuuza Wayne Rooney hasa kwenda Chelsea.

Tayari Man United imezitupa chini ofa mbili za Chelsea za kutaka kumchukua Rooney, lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 anataka kuandika maombi ya kuuzwa muda wowote kuanzia sasa kwa ajili ya kutimiza azma yake ya kuhama Old Trafford.

Hata hivyo, Neville anaamini kwamba kocha David Moyes analazimika kumbakiza Rooney kwa sababu ndiye mchezaji muhimu zaidi katika harakati za kuipatia Man United taji la 21 la ubingwa wa Ligi Kuu England.

Neville anaamini kwamba kama Moyes atamuuza Rooney, basi atalazimika kumnunua mchezaji mwenye kiwango cha juu sana kwa ajili ya kupata mbadala.

“Rooney ni mchezaji muhimu sana. Ni bingwa na ni mtu ambaye anaweza kukupatia ubingwa.

Manchester United haipaswi kumuuza kwenda Chelsea, labda kama wakimnunua mchezaji kama Gareth Bale au Cristiano Ronaldo,” alisema Neville.

“Ukiwa na Rooney ujue una dhahabu, mtu ambaye amethibitisha uwezo wake kwa miaka sita, saba, hadi minane iliyopita. Mtu ambaye kila msimu anaonyesha mambo makubwa.

Ana mabao mengi na pasi nyingi za mabao kwa kila msimu. Hata katika msimu uliopita alikuwa hivyo hivyo ingawa hakuwa katika msimu mzuri.

“Atakupa kila unachotaka na hawezi kushusha kiwango chake katika mazoezi. Umuhimu wa Rooney ni mkubwa.

Ni mtu ambaye katikati ya Oktoba wakati uko pointi nne nyuma na inabidi uende kucheza na Chelsea kisha Arsenal, atakaa mbele ya viungo wake wawili na kufanya kila anachoweza, akipigwa viatu lakini huku akiandaa mabao na kufunga.

“Msiidharau thamani ya Rooney kwa mafanikio ya Manchester United katika kipindi cha miaka minane iliyopita na jinsi ambavyo anapendwa na wachezaji wenzake.


Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive