Saturday, 18 April 2015

Chama cha ACT chaitaka serekali kutoa taarifa za uchunguzi wa ajali zinazo tokea mara kwa mara.

li kupunguza ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na wananchi kupata ulemavu,chama cha ACT wazalendo kimeitaka serekali kutoa taarifa ya tume ya uchunguzi wa ajali za barabarani zilizo fanyiwa utafiti ili kuweza kutafuta namna yakutatua matatizo ya ajali za mara kwa mara.
 akiwahutubia mamia ya wakazi wa manispaa ya Singida na viunga vyake  kwenye mkutano wa kunadi chama cha ACT kiongozi mkuu wa chama hicho Bwana. Zitto Kabwe ,amesema aliyekuwa waziri wa uchukuzi Dk Harsson Mwakyembe aliunda tume ya uchunguzi wa ajali na mpaka sasa majibu hayaja tolewa,jambo ambalo limekuwa likisababisha ajali kuendelea kutokea na kwa kipindi cha mwenzi Mach na April mwaka huu zaidi wa watu mianane wamesha poteza maisha kwa ajili ya ajali.
Katika hatua nyingine Bwana. Zitto Kabwe ameitaka serekali kuhakikisha inawabana wamiliki wa mabasi kote nchini  ,watoe  mikataba ya kazi   kwa madereva wao ili waweze kujulikana, kwa kufanya hivyo kuta punguza ajali ambazo siyo za msingi.
Awali mwenye kiti wa chama cha ACT Bi.Anna Mghwira na kada wa chama hicho Bwana  Selemani Msindi maarufu kwa jina la Afande Sele wamesema huduma nyingi  hasa za afya wakati wa zamani zilikuwa zikipatikana kulingana na uwezo wa serikali wakati ule, na kwasasa nchi imekuwa na utajiri mwingi wa madini ,kilimo na biashara,lakini cha kushangaza fursa hizo zimekuwa zikitumiwa na baadhi ya watu na kuwaacha wananchi wengi wakiwa masikini.
Share:

Follow Us

Random Posts

BTemplates.com

Powered by Blogger.
The Magazine

Facebook

Total Pageviews

Random Posts

Recent Comments

Recent Posts

Popular Posts

Blog Archive