Majonzi yalitawala shughuli hiyo hasa baada ya miili hiyo
kupokelewa katika viwanja vya shule ya msingi kibirizi kabla ya ndugu
kukabidhiwa tayari kwa maziko huku mwili wa Mwalim Elieza Mbwambo
ukisafirishwa kwenda moshi kwa maziko .
Akitoa salam za rambirambi mkuu wa mkoa wa kigoma Luten Kanal
Mstaafu Issa Machibya amewataka wafiwa na wananchi kuchukulia tatizo
hilo kama ni tukio la ajali ya kawaida na kwamba msiba huo ni mzito.
Kwa upande wao viongozi wa dini Shekh Moshi Guoguo kutoka Bakwata
na mchungaji Emmanuel Mtoi wa kanisa la KKKT wakitoa mawaidha katika
msiba huo, wamewataka waumini wa dini mbalimbali kujiandaa kwa kuwa kila
mwanadamu ataonja mauti kwa wakati wake na kwamba imani za kishirikina
zisihusishwe katika msiba huo.





