Maofisa zaidi ya 30 kutoka mamlaka ya chakula na dawa na baraza la Famasi Tanzania
wamekamata ghala lenye dawa za serikali,zilizopigwa marufuku na zilizokwisha muda wake wa matumizi zenye thamani ya shilingi milioni 97 zikiwa zinamilikiwa na mfanyabiashara wa jijini mwanza CHARLES MBUSIRO kinyume cha sheria.
wamekamata ghala lenye dawa za serikali,zilizopigwa marufuku na zilizokwisha muda wake wa matumizi zenye thamani ya shilingi milioni 97 zikiwa zinamilikiwa na mfanyabiashara wa jijini mwanza CHARLES MBUSIRO kinyume cha sheria.
Ghala hilo lililopo eneo la ilemela jijini mwanza limekutwa likiwa
limesheheni zaidi ya 120 za dawa ambazo ni sawa na tani 42 zikiwemo dawa
za serikali za Kenya na Uganda, dawa za misaada, dawa zilizopigwa
marufuku nchini kama vile klorokwini ya sindano, amodiaquine na gripe
water -dawa nyingine zilizokutwa ndani ya ghala hilo na kwenye duka lake
la dawa lililopo Natta barabara ya nyerere ni pamoja na ambazo
hazijasajiliwa na TFDA na azisizoruhusiwa kuuzwa kwenye maduka ya dawa.
Meneja wa usalama wa dawa wa TFDA Kissa Mwamwitwa ndiye aliyeongoza
zoezi hilo liliendeshwa chini ya usimamizi mkali wa askari polisi wenye
silaha za moto.
Baadhi ya maofisa wanaotekeleza operesheni hiyo, wakiwemo
wanasheria kutoka TFDA na baraza la famasi tanzania pamoja na meneja wa
mamlaka hiyo kanda ya kati Florent Kyombo wakizungumzia tukio hilo
wamesema taratibu za kisheria zinafanyika ili kumfikisha mahakamani
mtuhumiwa.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kahasa ilemela Richard Peter
alikuwa shuhuda wakati maofisa hao wa TFDA, baraza la famasi tanzania na
askari polisi walipokuwa wakitekeleza zoezi hilo kwenye ghala la dawa
ambalo linasemekana bado halijasajiliwa na TFDA huku mmliki wake charles
mbusiro akitoroka kwa kuruka ukuta na kutokomea kusikojulikana.





